Kuhusu Sisi
Tuna huduma kuu mbili; moja ni ya udalali (kutafutia wateja nyumba za kupanga) na ya pili ni program ya kutunza kumbukumbu za mchakato mzima wa kupangisha nyumba ikizingatia mmiliki wa nyumba, nyumba yenyewe, mpangaji, mkataba wa nyumba pamoja na makusanyo ya kodi ya nyumba.
Maono (Vision)
Kuwa watoaji namba moja Tanzania wa program ya kusimamia wapangaji na mikataba yao kwa kutumia teknolojia ya ubunifu ikiwa na lengo la kutoa huduma bora na ufanisi zaidi katika biashara ya kupangisha nyumba.
Dhamira (Mission)
Kurahisisha mchakato wa ukusanyaji kodi kwa wamiliki wa nyumba na kwa wakati, kupata taarifa sahihi za mpangaji na mkataba, kuhifadhi data salama. Tunalenga kuboresha mahusiano kati ya mwenye nyumba na mpangaji.
Malengo (Long-Term Plan)
Ifike muda jamii ya Kitanzania ihame kwenye kutumia daftari (counter book) na Excel File kwenye biashara ya kupangisha nyumba na badala yake itumie program yetu ya Pangisha.